Tarime. Wakazi 203 wa vijiji vinne vinavyozunguka mgodi wa Acacia North Mara wamesusia fidia iliyotolewa na mgodi huo kwa madai kuwa fedha wanazolipwa ni kidogo.
Mkuu wa wilaya ya Tarime Charles Kabeho, amesema leo Jumanne Machi 5, 2019 kuwa wananchi hao wamesusa kuchukua fidia hiyo wakidai fedha wanazolipwa hazilingani na thamani halisi ya ardhi na mazao yao.
"Mwitikio ni mdogo, wengi walijitokeza walipoona kiasi kilichoandikwa kwenye cheki zao hawakuridhika na kuamua kuacha kuchukua," amesema Kabeho.
Katika shughuli hiyo ililoanza jana Jumatatu mgodi huo ulitenga zaidi ya Sh3.8 bilioni kwa ajili ya kulipa fidia kwa vijiji vya Mjini kati, Nyakunguru, Nyamichele na Nyangoto.
Mkuu wa mkoa wa Mara, Adam Malima amesema baada ya kutoa taarifa hiyo kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Mara pamoja na Waziri wa Madini Doto Biteko wameamua kwenda Nyamongo ili kujua tatizo ni nini.
Endelea kufuatilia Mwananchi kujua kitakachojiri