Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wakulima wataka Serikali ya Tanzania kuwalipa Sh36 bilioni

76411 Wakulima+pic

Thu, 19 Sep 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Wasambazaji wa pembejeo za wakulima nchini wamemweleza Waziri wa Kilimo,  Japhet Hasunga hali ngumu wanayokumbana nayo kutokana na Serikali kutowalipa Sh36.9 bilioni.

Mwenyekiti wa Chama cha Ushirika cha Wazalishaji, Wasambazaji wa pembejeo za Kilimo na Mifugo, Gerald Mlenge ametoa kauli hiyo leo Septemba 19, 2019 kwenye mkutano wa wadau wa kilimo mjini Dodoma.

"Wenzetu 13 wameshatangulia mbele za haki, tunaomba fedha zetu Sh36.9 bilioni tulipwe kama kuna makosa kwa nini tusipelekwe katika vyombo vya dola, tusaidie kuonana na Waziri Mkuu (Kassim Majaliwa)tumwambie," amesema Mlenge.

Amesema kumekuwa na ucheleweshwaji wa wa kulipwa madai jambo linalowakatisha tamaa na baadhi wanapoteza maisha kwa sababu ya mawazo.

Hata hivyo, Hasunga ametaja sababu za kuchelewesha malipo hayo kuwa ni udanganyifu kwa kuwa kulikuwa na malipo hewa asilimia 80.

Waziri huyo amesema wakati wowote Serikali  itawafikisha mahakamani waliofanya udanganyifu huo ili sheria ichukue mkondo wake.

Pia Soma

Advertisement
 

Chanzo: mwananchi.co.tz