Nairobi, Kenya.Wakulima nchini Kenya wameionya Serikali dhidi ya uagizaji wa mahindi ili kutosheleza mahitaji ya bidhaa hiyo nchini humo.
Wakulima hao wamesema hawatakubali wizara ya kilimo kuagiza mahindi kwa kuwa hatua hiyo itawaharibia soko.
Wakulima hao pia wameitaka Serikali kusaidia wakulima badala ya kuwatajirisha wachache.
Aidha, wakulima hao wametaka kuwa na uwakilishi kwenye kila jukwaa linalozungumzia masuala ya kilimo.
Wamesema wasagaji wa unga wamekuwa wakitoa bei nzuri kwa mahindi yao pamoja na wafanya biashara wa kibinafsi kuliko Serikali.
Juzi gunia moja la kilo 90 lilikuwa likiuzwa kwa Sh 3,200.