Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wakulima vijana kushindania treka kwa mfumo huu

Waziri Bashe Aonya Kilimo Cha WhatsApp, Instagram Wakulima vijana kushindania treka kwa mfumo huu

Fri, 8 Sep 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Akipokea trekta lililokabidhiwa kwa Serikali kutoka kampuni ya Kimataifa ya wauzaji wa matrekta ya JOHN DEERE, Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema ili kuwakabidhi vijana trekta hilo umeandaliwa utaratibu wa kutangaza mashindano ili kumpata mshindi.

Bashe ameeleza kuwa utaratibu huo wa kumpata mshindi utahusisha mashindano ya vikundi vya vijana ambavyo vitatakiwa kuwasilisha andiko la wazo la biashara wanayotaka kufanya katika sekta ya Kilimo kuendana na matumizi na uhitaji wa trekta hilo.

“Mchakato huo utakuwa transparent tutashirikiana na John Deere, wizara ya Kilimo na AGRA kwa ajili ya kuendesha hayo.....Kikundi cha vijana kitakachoshinda kitakabidhiwa trekta". Amesema Waziri Bashe

Makabidhiano ya trekta hilo yamefanyika katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Dar es Salaam unapofanyika mkutano wa Mifumo ya Chakula Afrika 2023 (AGRF).

Chanzo: www.tanzaniaweb.live