Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini, Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu amewaagiza Wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini wilayani Songea, kuzingatia matumizi ya vifaa vyenye ubora na kuongeza nguvu kazi ili miradi hiyo ikamilike kwa muda uliopangwa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini, Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu amewaagiza Wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini wilayani Songea, kuzingatia matumizi ya vifaa vyenye ubora na kuongeza nguvu kazi ili miradi hiyo ikamilike kwa muda uliopangwa. Balozi Kingu pia amewataka Wakandarasi kufanya kazi kwa weledi na kuzingatia usalama wa miradi wanayoitekeleza ili azma ya Serikali kuhakikisha inawanufaisha wananchi iweze kutimizwa. -