Wafanyabiashara wa soko la Kariakoo wameiomba Serikali iwasilishe hoja ya kuondoa Sheria ya usajili wa stoo kwa hati ya dharura bungeni.
Wamesema kwa kuwa Serikali imewahi kufanya hivyo kwa nyakati tofauti ni muhimu sasa sheria hiyo ambayo ndio imewasababishia kufunga biashara iondolewe "Hii ni sheria kandamizi tumeziona Sheria nyingi zimeondolewa, hii mkaifute kwa hati ya dharura,"amesema Abraham Maghembe.
Mfanyabiashara huyo amesema kutokana na mlolongo wa kodi za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ambazo zinawafanya kuiona Tanzania chungu katika Uwekezaji huku nchi ambazo hazina bandari zikinufaika na bandari ya zilizopo Tanzania.