Menu ›
Biashara
Mon, 12 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Serikali imesema inaendela kutekeleza mikakati mbalimbali ya kuhakikisha viwanda vingi vinaanzishwa nchini vikiwemo viwanda vya kutengeneza pikipiki.
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Exaud Kigahe ameitaja mikakati hiyo kuwa ni pamoja na kuweka mazingira bora ya biashara na uwekezaji na kujenga miundombinu wezeshi kwa ajili ya ujenzi wa viwanda hivyo.
Kigahe ametoa kauli hiyo Bungeni jijini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa jimbo la Kigoma Mjini, Kilumbe Ng’enda aliyeuliza ni nini mpango wa Serikali katika kuanzisha kiwanda cha kutengeneza pikipiki nchini.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live