Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Vituo vya kuhifadhia ndizi,viazi kuanzishwa

A60462464e9c88cb18879015938bb509 Vituo vya kuhifadhia ndizi,viazi kuanzishwa

Tue, 3 Nov 2020 Chanzo: habarileo.co.tz

SERIKALI inajipanga kuboresha kilimo cha ndizi na viazi kwa kuwa na vituo vya kuhifadhia mazao hayo vyenye thamani ya Sh milioni 300 Vifaa hivyo vya kuhifadhia mazao vitakuwa maeneo ya Meru, Kisii na Nyandarua,. Kuwepo kwa vituo hivyo kunatarajiwa kusaidia wakulima wadogo kupunguza hasara walizokuwa wakipata kutokana na kutokuwa na maeneo ya kuhifadhia mazao.

Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Biashara,Viwanda na Ushirikiano, Patrick Wainaina, ambaye pia ni mbunge wa Thika Town alisema mradi huo tayari umetengewa fedha na unapaswa kukamilika kwa wakati.

“Hatutaki kuona watu wachache wakitumia vibaya fedha hizo na kuua ndoto za wakulima,kupata maeneo ya kuhifadhia mazao “alisema akiwa Kisii katika ziara ambayo waliandamana na wajumbe wengine wa kamati hiyo Andrew Mwadime (Mwatate), Jared Okello (Nyando) na mwenyekiti wake Ali Haji na Gure Anab.

Licha ya kuhakikisha usalama wa mazao ya wakulima wa viazi na ndizi ,kutakuwa na kituo cha kuchakata bidhaa na kupanua huduma ikiwemo kuratibu usafirishaji na masoko.

Kituo kwa ajili ya wakulima wa ndizi wa Kisii kipo Kiamokama na kinajengwa kwa Sh. Milioni 100. Kwa sasa kituo hicho kimefikia asilimia 76.

Kituo kinajengwa pioa kwa ajili ya wakulima wa Meru na kitatumia Sh. milioni 100 . Kamati ilibaini kuwa uzalishaji bora wa ndizi na viazi unaweza kupatikana tu wakati Jimbo limekamilisha miradi hiyo muhimu.

Vituo hivyo vikikamilika maduka yatakuwa na mazao ya ziada, na hivyo kupunguza upotezaji wa mazao hayo.

Kaunti ya Nyandarua inachangia asilimia 33 ya bidhaa za viazi zinazozalishwa nchini Kenya. Mnyororo wa thamani ya viazi, moja kwa moja, unasaidia familia za wakulima 131,697 katika kaunti hiyo .

Chanzo: habarileo.co.tz