Menu ›
Biashara
Tue, 4 Oct 2022
Chanzo: Eatv
Vijiji kumi na mbili katika halmashauri ya Mtwara vinatarajiwa kupitishwa bomba la gesi asilia la lenye urefu wa kilomita 35
Wananchi wa vijiji hivyo wametakiwa kutoa ushirikiano kwa shirika la maendeleo ya petroli Tanzania, (TPDC) kwa ajili ya kufanya tathimini ya mali, na kulipwa fidia zao, kwa ajili ya kuanza utekelezaji mradi huo.
Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Moma kata ya Moma katika kutambulisha mradi huo Mkuu wilaya ya hiyo Dustan Kyobya, akawataka wananchi kupokea mradi huo na kutoa ushirikiano wa kutosha wakati wa zoezi hilo
Chanzo: Eatv