Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Vigogo sekta ya nishati EAC wakutana Arusha

Mitungi Nya Gesi Bei.png Vigogo sekta ya nishati EAC wakutana Arusha

Wed, 14 Feb 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Makatibu Wakuu wanaosimamia Sekta ya Nishati katika Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wamekutana jijini Arusha katika mkutano wa 16 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Nishati la EAC unaoendelea jijini humo.

Mkutano huo ambao ulitanguliwa na mkutano wa Wataalam uliyofanyika tarehe 12 Februari 2024, umepitia na kujadili utekelezaji wa maamuzi na maelekezo ya Baraza la Mawaziri la Jumuiya. Vilevile umepokea na kujadili taarifa za maendeleo ya sekta ya nishati katika maeneo ya umeme, mafuta na nishati jadidifu.

Katika hotuba yake ya ufunguzi, Mwenyekiti wa Mkutano huo ambaye pia ni Katibu Mkuu anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki katika Jamhuri ya Kenya Bw. Abdi Dubati ameeleza kuwa mkutano huo ni mwendelezo wa jitihada za Wakuu wa Nchi wanachana wa Jumuiya, za kuhahikisha sekta ya nishati inaimarika ili kuchagiza maendeleo ya Jumuiya kutokana na mchango wake mkubwa katika kuvutia wawekezaji, kukuza biashara na uzalisha wa bidhaa viwandani.

“Nitoe rai kwetu sote tuliopata nafasi na kuaminiwa kusimamia maendeleo ya sekta hii muhimu kuwa tujidhatiti katika kutoa michango na kushirikishana uzoefu wetu ili kwa pamoja kama Jumuiya tupige hatua katika upatikanaji wa nishati ya kutosha, endelevu na salama kwa maendeleo ya Jumuiya yetu”. Alisema Dubati.

Kwa upande wake kiongozi wa ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huo ambaye pia ni Katibu Mkuu Wizara ya Nishati Mhandisi Felchesmi Mramba akizungumza kwenye ufunguzi wa mkutano huo ameleeza kuwa kikao hicho kinatoa fursa ya kuunganisha nguvu na kuweka mikakati ya pamoja katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya nishati ikiwemo umeme.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live