Menu ›
Biashara
Thu, 29 Feb 2024
Chanzo: Habarileo
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Kariakoo, Martin Mbwana amekiri kuwepo na changamoto ya utoaji risiti za kielektroniki maarufu kama EFD kutokana na mifumo kutokuwa rafiki kwa wafanyabiashara hao.
Mbwana ameyasema hayo kwenye Jukwaa la Kodi na Uwekezaji Februari 28, 2024 jijini Dar es Salaam.
Jukwaa hilo lililobeba kaulimbiu isemayo Maboresho ya Sera katika Uwekezaji, Ukusanyaji wa Mapato ya Ndani na Ukuaji wa Uchumi Jumuishi lilifunguliwa Februari 27, 2024 na Makamu wa Rais Dk Philip Mpango kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.
Chanzo: Habarileo