Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba amesema Serikali itaanza kutoza ushuru wa bidhaa kwa kiwango cha asilimia 10 katika magari ya abiria yanayoingizwa nchini yanayozidi umri wa miaka mitano (magari chakavu).
“Hatua hiyo inakuja ili kuwianisha na magari mengine yanayofanana yanayotozwa ushuru huo. Magari hayo ni yale yanayotambuliwa kwa H.S Codes 8702.20.22, 8702.20.29, 8702.20.99, 8702.30.22, 8702.30.29, 8702.30.99, 8702.40.22, 8702.40.29 na 8702.40.99,”amesema
Dk Nchemba ameyasema hayo leo Alhamis Juni 15, 2023 akiwasilisha hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka wa fedha 2023/2024.