Mradi mkubwa wa upanuzi wa bandari ya Tanga umefikia asilimia 26 wa ujenzi wake huku ukitarajiwa kukamilika Oktoba mwaka huu
Akizungumza na waandishi wa habari jana katika maonesho ya TANZFOODS,Mhandisi Hamis kipalo alisema mradi huo upo nyuma ya muda kutokana na changamoto mbalimbali ikiwemo ya ugonjwa wa Covid 19 iliyosababisha nchi nyingi kufunga mipaka
"Ugonjwa wa Covid 19 ulisababisha vifaa vya ujenzi kutoingia nchini kutokana na nchi nyingi kufunga mipaka yao"alisema Mhandisi Kipalo
Aliongeza kuwa mradi huo ukikamilika utaleta manufaa makubwa kwa nchi katika kuongeza ufanisi wa bandari kutoka tani laki saba na nusu hadi tani Milioni 30
"Uwezo wa bandari utaongezeka na pia itasaidia biashara katika ukanda wa kaskazini na Afrika Mashariki "alisema Mhandisi Kipalo
Naye Afisa uhusiano wa bandari ya Tanga,Adam Shindo alisema ushiriki wao katika maonyesho hayo ni kusogea karibu na wateja wao nakutumia fursa hiyo kwa kujitangaza zaidi
"Kilichotuleta hapa ni kusogea karibu na wateja wetu na kuwaelezea maendeleo ya mradi,upanuzi wa bandari ya tanga "alisema Shindo
Mradi huo unatekelezwa na kampuni ya CHEC kutoka China na kusimamiwa na Mhandisi mshauri kutoka Denmark ikishirikiana na kampuni ya Kitanzania Anova