Menu ›
Biashara
Tue, 25 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega amewataka Wawekezaji wote waliopewa vitalu katika mashamba ya Serikali kuhakikisha wanaendeleza vitalu hivyo kwa kufanya ufugaji wa kisasa huku akiwaelekeza kuondoa vichaka katika vitalu hivyo.
Waziri Ulega ameyasema hayo wakati wa ziara yake Wilayani Misenyi mkoani Kagera.
Amesema mwekezaji ambaye anaona hawezi afanye ushirikiano na Wataalam wanaoweza kumsaidia kufuga kisasa au aondoke ili eneo hilo wakabidhiwe watu wengine wenye uwezo wa kuliendeleza.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live