Ujenzi wa kiwanja cha ndege cha Nduli mkoani Iringa, umefikia asilimia 82 na ukitarajiwa kukamilika mwishoni wa Desemba 2023.
Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, David Kihenzile amesema hayo baada ya kutembelea kiwanja hicho ambacho kimegharimu zaidi ya Sh63.7 bilioni, ili kuangalia maendeleo ya ujenzi wake.
"Ujenzi wa kiwanja hiki cha ndege kitasaidia kuinua uchumi wa wakazi wa mkoa wa Iringa kupitia sekta mbalimbali ikiwemo utalii kwakuwa unaunganisha dunia na Hifadhi ya Taifa ya Ruaha," amesema Kihenzile
Pia ameeleza Serikali inajenga barabara ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha kwa kiwango cha lami lengo ikiwa ni kufanya utalii unakuwa wa kisasa.