Uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Songwe umesema zaidi ya tani 1,000 ya zao la ufuta zinatarajia kuuzwa katika mwendelezo wa mnada kwa njia ya stakabadhi ghalani ambao unawahusisha wakulima vyama vya msingi vya ushirika pamoja na makampuni makubwa ya ununuzi ya kimataifa.
Uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Songwe umesema zaidi ya tani 1,000 ya zao la ufuta zinatarajia kuuzwa katika mwendelezo wa mnada kwa njia ya stakabadhi ghalani ambao unawahusisha wakulima vyama vya msingi vya ushirika pamoja na makampuni makubwa ya ununuzi ya kimataifa. Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Cpa Cecilia Kavishe amesema licha ya mfumo huo kulenga kumkomboa mkulima lakini pia shabaha nyingine kuweka sawa takwimu za uzalishaji wa zao, kuongeza mapato ya halmashauri hiyo pamoja na kuzuia mianya ya unyonyaji kwa wakulima.