Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Uchumi wa Tanzania Umepanda

Uchumi Kupanda Uchumi wa Tanzania Umepanda

Wed, 5 Jan 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Takwimu zilizotolewa na Ofisi ya Taifa Takwimu (NBS) zinaonesha kuwa Uchumi wa Tanzania umekuwa kutoka asilimia 4.4 hadi asilimia 5.2, katika kipindi cha cha robo ya tatu ya mwaka 2021.

Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi Takwimu za Uchumi Daniel Masolwa, wakati akizungumza na waandishi wa Habari Jijini Dodoma.

Masolwa, amefafanua kuwa Shughuli za Ujenzi, kilimo na uchimbaji wa madini ni kati ya sababu za ukuaji wa Uchumi wa asilimia 5.2.

Kwa mujibu wa Masolwa, nchi jirani za Afrika Mashariki zilizotoa ripoti zao ni Rwanda ambayo uchumi wake umekuwa kwa asilimia 10.1 na Uganda ambayo uchumi wake umekuwa kwa asilimia 3.8.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live