Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

UDSM waongeza muda wa juisi ya miwa kutumika

65177 Pic+miwa

Tue, 2 Jul 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Umewahi kufikiria jinsi ya kuhifadhi juisi ya miwa ambayo inapaswa ikikamuliwa inywewe muda huohuo kwani ikikaa muda mrefu inapoteza ladha yake.

Chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) nchini Tanzania imelifikiria hilo na kuja na mbinu mpya ya kuitunza kwa zaidi ya mwezi mmoja na ikawa na ladha yaje ileile kwenye maonyesho ya 43 ya kimataifa yanayoendelea Jijini Dar es Salaam, Tanzania.

Mwanafunzi wa shahada ya umahiri kutokana idara ya chakula na sayansi wa UDSM Boniface Joshua amesema alifikiria ni kwa namna gani anaweza kutunza juisi ya miwa.

Amesema baada ya kutafakari kwa kina na kukaa maabara kujaribu hiki na kile akabaini akichanganya kitunguu maji na majani ya mti wa mlonge vina wingi wa vihifadhi chakula.

Amesema kwa kutumia vyakula hivyo ameweza kurefusha muda wa kukaa juisi ya miwa kutokana siku sifuri hadi zaidi ya siku 30.

Amesema pia wakati anatafiti alibaini juisi ya miwa inayotengenezwa mtaani ina upungufu wa viini lishe kama vitamini A na C  na haina baadhi ya madini muhimu katika mwili wa binadamu kama zink ambayo ni muhimu kwa afya ya uzazi, China, potasiam na sodiam.

Pia Soma

"Hivyo juisi hiyo ukiichanganya na vitunguu maji na majani ya mlonge kisha ukaitayarisha bila kuongeza kitu kingine ina uwezo wa kudumu kwa zaidi ya siku 30" amesema Joshua.

Huku akionyesha juisi ya miwa iliyopo ndani ya chupa ukiwa imefungwa vema amesema kuwa hata ikitingishwa haitoki povu kwa kuwa ipo salama.

Chanzo: mwananchi.co.tz