Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

"Tutaendeleza uzalishaji wa viwanda Barani Afrika" Katibu Doto James (+picha)

Picha 0003 660x400 "Tutaendeleza uzalishaji wa viwanda Barani Afrika" Katibu Doto James (+picha)

Fri, 30 Apr 2021 Chanzo: millardayo.com

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Doto James amesema Tanzania  imedhamiria  kukuza na kuendeleza uwezo wa uzalishaji  wenye tija na ufanisi viwandani ili kuongeza ushindani katika soko la ndani, kikanda na kimataifa  ili kukuza uchumi na maendeleo endelevu.

Katibu Mkuu huyo aliyasema hayo alipokuwa akifungua kongamano la siku mbili kwa njia ya mtandao linalohusu mikakati oanishi ya kuendeleza uwezo wa uzalishaji viwandani nchini linalofanyika kuanzia tarehe 29 na 30 Aprili, 2021 katika hoteli ya Morena jijini Dodoma. 

Akiongea katika kongamano hilo, Katibu Mkuu aliwasisitiza washiriki kujikita katika kuainisha mikakati oanishi katika sera za viwanda, biashara, uwekezaji na masoko itakayoendeleza njia za uzalishaji mpya na matumizi bora ya njia za uzalishaji zilizopo ili kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya mwaka 2025 na Malengo ya Maendeleo endelevu. 

Aidha, Doto alisema kongamano hilo linafanyika wakati muafaka ambapo mapendekezo yatakayotolewa yatachangia kwa kiasi kikubwa maboresho ya sera zinahusu maendeleo ya Sekta ya Viwanda na Biashara zinazopitiwa na wizara kwa sasa. 

Aidha Bw. Doto alisema Wizara ya Viwanda na Biashara inatambua hatua mbalimbali zinazotekelezwa na sekta ya uzalishaji katika kukuza uchumi na inaendelea kuchukua hatua mbalimbali katika kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta hiyo ili kuongeza uzalishaji, mauzo ya nje, mazao ya kilimo pamoja kuimarisha uzalishaji wa sekta nyingine.

Doto pia aliishukuru UNCTAD na Ofisi za Umoja wa Mataifa zilizopo nchini  kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kutoa msaada wa kitaalamu  katika utekelezaji wa miradi mbalimbali katika sekta ya viwanda na biashara  hususani  Mradi wa Mikakati Oanishi wa Kuendeleza Uwezo wa Uzalishaji barani Afrika.

“Tanzania inatekeleza Mradi wa Mikakati Oanishi wa Kuendeleza Uwezo wa Uzalishaji Viwandani barani Afrika ili kutathmini uwezo wa uzalishaji, jitihada za maendeleo, changamoto zilizopo na njia sahihi za kuzitatua” Doto James

 Kongamano hilo kwa njia ya mtandao, lilihudhuriwa na wawakilishi wa Umoja wa Mataifa,  Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo(UNDP), Shirika Kongamano la Umoja wa Mataifa kuhusu Maendeleo ya Biashara (UNCTAD),  waliopo Tanzania, Geneva na Vienna, Balozi wa kudumu wa Tanzania umoja wa Mataifa Geneva, Watumishi kutoka Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali ya Tanzania  bara na Zanzibar pamoja na Sekta Binafsi.



 

Washiriki hao walipata fursa za kuwasilisha mada mbalimbali na kufanya majadiliano yaliyohusu kuendeleza uwezo wa uzalishaji viwandani na ukuzaji wa sekta binafsi.
Chanzo: millardayo.com