Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Trump apiga dongo Elon Musk kununua Twitter

9F192D7E 82A3 4CCF 82B3 5D55C76FC471 1140x640.jpeg Trump apiga dongo Elon Musk kununua Twitter

Sat, 29 Oct 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Rais wa zamani wa Marekani, Donald Trump amefurahia hatua ya kampuni ya Twitter kununuliwa na bilionea Elon Musk, akisema kampuni hiyo maarufu ya mtandao wa kijamii hivi sasa ipo mikononi mwa mtu mwenye akili timamu.

Musk amekamilisha ununuzi wa kampuni hiyo Oktoba 27, 2022 kwa malipo ya dola bilioni 44, baada ya miezi kadhaa ya tetesi na minong’ono juu ya kufanyika kwa biashara hiyo. 

Kupitia mtandao wake mwenyewe, ujulikanao kama Truth Social, Trump ametumia maneno makali, akisema “Ninafurahi sana kuwa Twitter haitaendeshwa na wendawazimu wenye sera za mrengo wa kushoto.” 

Hatua ya Elon Musk, kuimiliki Twitter imesababisha hofu miongoni mwa wanaharakati kuwa itageuzwa jukwaa la unyanyasaji na habari za kupotosha, kwa hoja kwamba Musk mwenyewe anajulikana kwa kuwashambulia watumiaji wa mtandao huo. 

Chanzo: www.tanzaniaweb.live