Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Tanzania yazindua mifumo mitatu kuendeleza sekta ya kilimo

70582 Tz+pic

Fri, 9 Aug 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Bariadi. Serikali ya Tanzania imezindua mifumo mitatu yatakayotumika kuendeleza, kuboresha na kuongeza tija katika sekta ya kilimo.

Mifumo hiyo imezinduliwa jana Alhamisi Agosti 8, 2019 na Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa katika viwanja vya Nyakabindi wikayani Bariadi mkoani Simiyu wakati wa kilele cha maonesho ya Nanenane kitaifa.

Waziri wa Kilimo, Japheth Hasunga alitaja mfumo wa kwanza ni ule wa masoko inayoweka uwazi na kuunganisha wakulima na wanunuzi wa ndani na nje ya nchi.

"Mfumo wa pili ni wa usimamizi wa biashara ya sekta ya kilimo kwa njia ya kielektroniki," alisema Hasunga

Waziri Hasunga alitaja mfumo wa tatu ni wa usajili na kanzi data ya wakulima inayoonyesha idadi yao, aina ya mazao wanayolima, ekari wanazolima na matarajio ya mavuno yao kila msimu.

Akizindua mifumo hiyo, Waziri Mkuu Majaliwa aliagiza michakato yote yanayohusu maendeleo ya sekta ya kilimo kushirikisha wadau wote kuanzia wakulima kupitia vyama vyao vya msingi (Amcos),  taasisi za fedha, wataalam, taasisi za kilimo na viongozi kuanzia ngazi ya msingi.

Pia Soma

"Usajili wa wakulima uanze mara moja ili kurahisisha utekelezaji wa mifumo mengine ikiwemo utoaji wa elimu, huduma ya ugani na mfumo wa malipo kwa njia ya kibenki kuondoa mazoea ya malipo ya fedha taslimu," aliagiza Waziri Mkuu

Kiongozi huyo aliziagiza mabenki na taasisi zote za kifedha kuhakikisha huduma zao zinawafikia wakulima vijijini.

"Mabenki yafungue matawi au kuweka mawakala hadi vijijini kuwezesha wakulima kufungua akaunti na kupata huduma za kibenki ili kuongeza usalama wao na fedha zao wakati na baada ya mavuno," alisema

Alitoa mfano wa tukio la kukuta boksi iliyojaa mamilioni ya fedha katika jengo la mabati ya moja ya chama cha msingi cha ushirika wilayani Bariadi walikokuwa wanalipwa wakulima wa zao pamba.

"Viongozi wale wa Amcos watafanya kazi ile ya malipo karibia kutwa nzima na fedha zikibaki zilale kwenye lile jengo la bati. Wakulima wale wangekuwa na akaunti   wangelipwa kwa njia ya benki; siyo tu ingewaondolea usumbufu wa kupanga foleni kutwa nzima, bali pia ingewahakikishia usalama wao binafsi na fedha zao," aliongeza

Waziri Mkuu Majaliwa alimwagiza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka na wenzake wa mikoa mingine inayolima pamba kuhakikisha ulinzi wa kutosha wakati wote wa ununuzi na malipo ya wakulima kupitia Amcos zao.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz