Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Tanzania yataja sababu za kupungua kwa mauzo ya nje

64262 Mauzo+pic

Tue, 25 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amesema kupungua kwa mauzo yanayotokana na sekta ya uvuvi nchini mwaka 2018 yanatokana na operesheni ya kuondoa uvuvi haramu.

Mpina ametoa kauli hiyo leo Jumanne Juni 25, 2019 wakati akijibu hoja zilizotolewa na wabunge waliochangia bajeti ya Serikali kwa mwaka 2019/2020 ya Sh33.1 trilioni.

Akijibu hoja ya kushuka kwa mapato yanayotokana na mauzo nje ya Tanzania, Mpina amesema takwimu zinaonyesha  katika sekta ya uvuvi mauzo kwa mwaka 2018 yalikuwa ni dola za Marekani milioni 158 lakini mwaka 2017 ilikuwa ni dola za Marekani milioni 193.

“Na miaka yote ile inacheza katika dola za Marekani 160. Lakini nawaambia wabunge tumefanya kazi kubwa mambo haya yametokana na operesheni za kuzuia uvuvi haramu wa mabomu,” amesema.

Mpina amesema hadi kufikia mwaka 2019 mauzo ya sekta hiyo yamefikia Dola za Marekani milioni 284 sawa na Sh654bilioni na kwamba haijawahi kutokea nchini.

Mwaka huu watakuwa wamenunua meli na kwenda kuvua bahari kuu na kwamba wamejipanga.

Pia Soma

Aidha, amesema wabunge wamelalamikia tozo ya asilimia 0.4  inayotozwa bahari kuu na kwamba katika kutatua hilo kesho Jumatano wanakutana na waziri wa upande wa Zanzibar anayeshughulikia uvuvi ili waweze kujadili na kutoka na uamuzi.

Chanzo: mwananchi.co.tz