Tanzania, Algeria na Nigeria, na nchi nyingine za Afrika ziko kwenye rada za makampuni mengi makubwa ya mafuta yenye biashara barani Ulaya ambayo yanajaribu kufunga mikataba katika bara hilo.
"Hadi sasa, makampuni makubwa ya mafuta na gesi BP, Shell, ExxonMobil na Equinor inayomilikiwa na serikali ya Norway yameonyesha nia yao ya kuondoka Urusi.
Wakati Total haitafanya uwekezaji wowote mpya," wataalam wa kampuni hiyo wanasem, Afrika ilitoa asilimia 18 ya gesi barani Ulaya iliyoagizwa kutoka nje katika muongo mmoja uliopita na sasa inajiandaa kuongeza sehemu hiyo.
"Uzalishaji wa gesi barani Afrika kwa sasa unatarajiwa kuanza kuongezeka katika nusu ya pili ya muongo huu wakati miradi mipya inakuja mtandaoni. Wimbi jipya la kuharakisha mradi linaweza kuchochea ukuaji huu."
Na anataja mifano kama vile Eni ya Italia ambayo itaharakisha mradi wake nchini Kongo na inalenga kusaidia kuleta vifaa Ulaya kutoka kwa miradi ya Algeria, Misri, Nigeria na Angola.
Kwa upande wao, Shell, Equinor na ExxonMobil wana mipango muhimu nchini Tanzania.