Menu ›
Biashara
Thu, 26 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Tanzania na Zambia zimesaini hati nane za makubaliano ya ushirikiano katika sekta mbalimbali ikiwemo sayansi, teknolojia na ubunifu, ulinzi, afya, gesi asilia, uwekezaji na biashara.
Makubaliano hayo yamesainiwa jana na kushuhudiwa na viongozi wa nchi zote mbili, Rais Hakainde Hichilema wa Zambia na Rais Samia Suluhu wa Tanzania ambao kwa pamoja wamesisitiza umuhimu wa makubaliano hayo kutekelezwa badala ya kutupwa kwenye makabati.
Kusainiwa kwa makubaliano hayo ni sehemu ya ziara ya kitaifa ya siku tatu ya Rais Samia Suluhu Hassan nchini Zambia ambayo imemalizika jana.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live