Wananchi wameaswa kutumia Taasisi ya Kiserikali ya Usuluhishi wa Malamiko na Taarifa za Kodi ‘TOST’ kwaajili ya kushughulikia changamoto wanazokutana nazo walipa kodi kuhusiana na taratibu za usimamizi wa Sheria za kodi na maamuzi mbalimbali ya Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA.
Wito huo kwa walipa Kodi umetolewa leo na Msuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi Bw. Robert Manyama wakati akizungumza na Wahariri na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam ambapo amesema taasisi hiyo uliyoundwa chini ya wizara ya fedha iliundwa ili wananchi waweze kupeleka malalamiko yao mbalimbali na yaweze kutatuliwa kwa haraka.
Usuluhushi wa malalamiko ya Kodi kwa wakati utaounguza kwa kiasi kikubwa pingamizi za kodi na migogoro ambayo isiyo na ulazima wa kupelekwa mahakamani” amesema Manyama.