Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imewatahadharisha wafanyabiashara kuepuka kufanya udanganyifu katika mfumo mpya wa ukusanyaji mapato kwa njia ya kielekroniki unaotegemewa kuanza kutumika mwezi Machi.
Akitoa elimu kwa wafanyabiashara katika Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera, Afisa elimu kwa walipa kodi mkoani Kagera amesema serikali inaendelea kuboresha mfumo huo na iko tayari kumuelimisha mfanyabiashara mahala popote na kwa wakati wowote.
“Ni mfumo mpya unaotarajiwa kuanza kutumika mwezi huu,” amesema. Mfumo huo unawataka wafanyabiashara kuepuka kufanya udanganyifu na kanuni zimeweka masharti ya adhabu ya Sh 250,000 kwa kampuni na Sh 75,000 kwa mtu binafsi kwa mwezi.