Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

TRA yasisitiza matumizi sahihi risiti za EFD

Efd Machineee.jpeg TRA yasisitiza matumizi sahihi risiti za EFD

Sun, 10 Dec 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

MAMLAKA ya Mapato Nchini (TRA), imewasisitiza wafanyabiashara kutambua kuwa matumizi sahihi ya Mashine za Risiti za Kielektroniki (EFD) ndio njia sahihi kwa wao kudhibiti ubadhirifu kwenye ofisi zao.

Kamishina wa Kodi za Ndani, Alfred Mregi ameeleza hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Geita mara baada ya watumishi wa TRA kutembelea na kusaidia makundi maalum.

Amesema mwamko wa matumizi ya EFD unaendelea kukua, lakini bado kuna watu hawatumii EFD, na wengine wapo wanatumia lakini si kwa usahihi hali inayofanya wafanyabiashara kukosa taarifa sahihi.

“Nitoe wito kwa wafanyabiashara wote kuviona vifaa hivi kwamba ni kwa ajili ya manufaa ya pande zote mbili, kwa sababu unapotumia mashine za EFD, kila unapouza na kutoa risiti, inakupatia tathimini sahihi.

“Lakini inakusaidia kutunza kumbukumbu ya bidhaa zako, kwa hiyo hata kama kuna ubadhirifu mtu hawezi kuufanya kwa sababu kumbukumbu zipo kwenye mashine.” Amesema na kuongeza;

“Watumishi wa TRA tunapokuja kupitia kumbukumbu zako kwa ajili ya kutoza kodi tunakukuta una kumbukumbu sahihi, kwa hiyo kodi ambayo itatozwa pale ni ile inayoendana na mapato yako.

“Lakini wanapokwepa kutumia hizi mashine zina athari kwa biashara zao, katika kukadilia kodi wanaweza wakalalamika kwamba wamekadiriwa kodi kubwa, kumbe suluhu ni kutumia mashine zile.”

Chanzo: www.tanzaniaweb.live