Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

TPDC yapata hasara ya Sh829.5 bilioni kwa miaka mitatu

39684 Kamatipic TPDC yapata hasara ya Sh829.5 bilioni kwa miaka mitatu

Mon, 4 Feb 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma.  Kamati ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma(PIC) imeyataja mashirika matatu yanayojiendesha kwa hasara likiwemo Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) ambalo limepata hasara ya Sh829.51 bilioni katika kipindi cha miaka mitatu.

Akisoma taarifa za kamati hiyo leo Jumamosi Februari 2, 2019 bungeni jijini Dodoma, mwenyekiti wa kamati hiyo, Dk Raphael Chegeni amesema mashirika mengine ni kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC) na Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC).

Amefafanua kuwa TPDC limekuwa likijiendesha kwa hasara kwa miaka mitatu mfululizo  kuanzia  2015 hadi 2016/17 na kwamba matumizi yamekuwa yakiongezeka ikilinganishwa na mapato yaliyokusanywa na kusababisha shirika kupata hasara.

Amefafanua kuwa mwaka 2014/15, TPDC ilipata hasara ya 297.71bilioni , mwaka 2015/16 hasara ya  Sh374.62 bilioni  na mwaka 2016/17 hasara ya Sh157.18bilioni

“Kupatikana kwa hasara ya muda mrefu kwa baadhi ya taasisi na mashirika ya umma kunachangia kwa kiasi kikubwa uendeshaji wa kusuasua kwa taasisi hizo kusababisha miradi mingi ya uwekezaji kushindwa kutekelezeka na kukamilika kwa wakati ili iweze kuleta tija iliyotarajiwa,” amesema.

 

 



Chanzo: mwananchi.co.tz