Mkurugenzi wa Bandari ya Dar es Salaam, Mrisho Mrisho, amesema wanafanya kazi kwa Saa 24 ikiwemo wikiendi kukabiliana na changamoto ya Mizigo kuchelewa kutoka ili kuhakikisha Meli zilizopo kwenye foleni zinatoka
Tamko hilo limetolewa siku chache tangu Mdau kudai kuna Mazingira ya Urasimu katika Bandari hiyo hali inayosababisha Mizigo kuchelewa kutoka, badala ya wiki moja au mbili wanalazimika kusubiri zaidi ya Miezi miwili
Mrisho anasema “Watanzania hasa wateja wetu wawe wanatuelewa kuwa kuanzia Oktoba na mwanzo wa Mwaka kuna ongezeko kubwa la Meli, ndio maana tuna ‘shift’ tatu ndani ya Saa 24 na tunaomba Meli ziendelee kuja kwa kuwa ndio Uchumi wa Taifa hili.”