Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imesema hakuna mgomo katika bandari hiyo na kwamba watumishi wote wanatimiza majukumu yao kikamilifu kwa kuzingatia ratiba za sehemu zao za kazi.
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imesema hakuna mgomo katika bandari hiyo na kwamba watumishi wote wanatimiza majukumu yao kikamilifu kwa kuzingatia ratiba za sehemu zao za kazi. TPA imetoa taarifa muda huu ikikanusha uvumi kuwa mgomo huo ulisababishwa na Mamlaka kusitisha mikataba ya baadhi ya watumishi. “Hakuna mtumishi yeyote wa Mamlaka aliyesitishiwa mkataba wake kwa sababu zozote zile,” imesema taarifa ya TPA.