Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

TBS yatakiwa kutoa majibu ya sampuli ndani ya siku moja

73570 Sampuli+pic

Fri, 30 Aug 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Waziri wa Viwanda na Biashara nchini Tanzania, Innocent Bashungwa amelitaka Shirika la Viwango nchini  (TBS) kutoa majibu ya sampuli ndani ya siku moja badala ya siku tatu hadi saba kwa sasa.

Bashungwa ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Agosti 30, 2019 wakati akizungumza na wafanyakazi wa shirika hilo.

Amesema mitaani kuna kero ya ucheleweshaji wa majibu ya sampuli zinazotumwa, kwamba takwimu alizonazo zinaonyesha ni siku tatu hadi saba au zaidi.

“Matamanio yangu ni kuona siku moja tu watu wanapata majibu yao. Sasa hivi tupo katika teknolojia tutoke kwenye siku tatu hadi saba kwa sababu TBS inategemewa na Watanzania hasa wafanyabiashara,” amesema Bashungwa.

Kuhusu wafanyabiashara wa nondo kulalamikia Wakala wa Vipimo (WMA), Bashungwa amesema atakutana na watendaji wa taasisi hiyo pamoja na TBS kwa ajili ya kuzungumza kwa kina kuhusu changamoto hiyo.

“WMA na TBS wote wapo chini ya wizara hii tutakaa na kuangalia yote yanayotakiwa ushirikiano kati yao ili kuondoa sintofahamu kwa umma. Lengo letu ni kuwawezesha wafanyabiashara si kuwasumbua,” amesema Bashungwa.

Pia Soma

Advertisement   ?
Jana katika kikao kilichoitishwa na TBS ilidaiwa hatua ya maofisa wa Wakala wa Vipimo (WMA) kwenda kinyume na matakwa ya shirika hilo la viwango ni moja ya kero katika  utekelezaji wa majukumu yao.

Wamedai maofisa wa WMA wakienda kufanya ukaguzi kwenye maeneo yao na kubaini nondo zimeongezeka urefu, wanakataa na kuwaeleza kuwa si kiwango kinachohitajika kisha kuwatoza faini.

Mkurugenzi wa TBS, Dk Yusuf Ngenya amesema wataongeza juhudi ili kuhakikisha majibu ya sampuli yanatolewa kwa wakati kama waziri alivyoeleza.

Chanzo: mwananchi.co.tz