Menu ›
Biashara
Tue, 15 Feb 2022
Chanzo: ippmedia.com
Taasisi ya utafiti wa uvuvi Tanzania TAFIRI inatarajia kufanya utafiti wa kutamba wingi wa samaki katika Bahari ya Hindi na Ziwa Tanaganyika utakaodumu kwa siku 30 kuanzia wiki ijayo.
Akitoa taarifa hiyo leo Mkurugenzi Mkuu wa TAFIRI, Ismael Kimirei amesema lengo ni kujua samaki waliopo na kuwa wamegawanyika kwa upana upi ili kuwavutia wawekezaji na kukuza uchumi wa bluu.
Amesema Bahari ya Hindi kwa mara ya kwanza inaingia katika utafiti huku Ziwa Tanganyika utafiti huo ulifanyika miaka 30 iliyopita.
Chanzo: ippmedia.com