Menu ›
Biashara
Thu, 18 Jan 2024
Chanzo: Millard Ayo
Jumla ya Tani 50000 za sukari zinatarajiwa kuingizwa Nchini kuanzia January 22,2024 kutoka nje ya Nchi ikiwa ni moja ya njia za kupunguza makali ya changamoto ya upungufu wa sukari ambao umejitokeza siku za hivi karibuni kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo mvua za Elnino.
Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Sukari Tanzania, Keneth Bengesi amesema hayo Jijini leo January 18,2024 wakati akiongea na Waandishi wa Habaaru juu ya hali ya uzalishaji wa sukari ilivyo mwaka huu na changamoto ambazo zimejitokeza na hatua mbalimbali ambazo wamechukua ili kukabiliana na changamoto hizo.
Chanzo: Millard Ayo