Mwenyekiti wa Machinga Soko la Kariakoo, Steven Lusinde amesema moja ya njia ya kuwasaidia wafanyabiashara wadogo maarufu kama Machinga wa soko la Kariakoo ni kuwapa nafasi ya kuingia kwenye masoko mapya yanayojengwa ili wafanye biashara zao kwenye mazingira mazuri
Mwenyekiti wa Machinga Soko la Kariakoo, Steven Lusinde amesema moja ya njia ya kuwasaidia wafanyabiashara wadogo maarufu kama Machinga wa soko la Kariakoo ni kuwapa nafasi ya kuingia kwenye masoko mapya yanayojengwa ili wafanye biashara zao kwenye mazingira mazuri Ameyasema hayo alipozungumza nasi leo ilipofika katika soko hilo kujua changamoto zao na namna ambavyo mikopo wanayopewa inawasaidia kuboresha biashara zao ambapo moja ya ombi lake kwa serikali ni kuomba maching wapewe kipaumbele katika masoko mapya yanayojengwa jijini Dar es Salaam.