Menu ›
Biashara
Thu, 9 Jun 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Umoja wa Ulaya (EU) umeridhia Kanuni zitakazolazimu simu zote zinazouzwa katika Umoja huo kuwa na 'Port' ya USB-C, uamuzi ambao ni pigo kubwa kwa Kampuni ya Apple yenye mfumo tofauti katika baadhi ya bidhaa zake.
EU imesema Kanuni hizo zinazotarajiwa kuanza kutekelezwa 2024 zinalenga kupunguzia wateja usumbufu wa kutumia Chaja tofauti katika vifaa vyao na kudhibiti uchafu wa kielektroniki kwa kuondoa ulazima wa kununua Chaja mpya kwa kila unaponunua simu.
Baada ya maridhiano hayo, Kanuni hizo zitahitaji kupitishwa na Bunge pamoja na Baraza la Ulaya.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live