Lindi. Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo Tanzania (Sido) limewapatia wafanyabiashara wadogo mkopo wa Sh43 milioni kwa ajili ya kuboresha mitaji yao.
Akizungumza jana Ijumaa Februari 21, 2020 meneja wa Sido Mkoa wa Lindi, Kasisi Mwita amesema shirika linatoa mikopo kwa wananchi kutoka mfuko wa Taifa wa kuendeleza wafanyabiashara (NEDF).
Mwita amesema hadi Desemba 31, 2019 mikopo 1,388 ya Sh1.9 bilioni imetolewa ambayo ni wastani wa Sh1.4 milioni kwa kila mtu.
Pia Soma
- Sudan Kusini yakwamisha vigogo EAC kukutana Tanzania
- Majaliwa: Uzalishaji mbegu za michikichi unaridhish
- Ulega alivyotatua kero ya wananchi kwa kumpigia simu bosi TFS
Amebainisha kuwa vikundi 48 vimepata mikopo, wanawake 534 wanaume 546 na kwamba waliopewa wanarejesha vizuri na kusaidia kupanda kwa ukopeshaji , “kwani kwa kipindi cha miaka minne Sh895.9 milioni zimewafikia wafanyabiashara 414.
Mkuu wa Wilaya Lindi, Shaibu Ndemanga amewataka wafanyabiashara hao kutumia mikopo hiyo katika shughuli walizopanga kuzifanya ili waweze kujikwamua kiuchumi.
Amewataka wafanyabiashara kuwa wabunifu ili waweze kurejesha mikopo yao kwa wakati.
Baadhi ya wafanyabiashara hao, Amina Halfani na Mustafa Hasani wameshukuru Sido kwa kuwapa mikopo yenye riba nafuu itakayosaidia kuinua mtaji wao.