Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Sh14 bilioni kutumika kuhamisha gereza la kilimo Songwe

Gereza Pic Data Sh14 bilioni kutumika kuhamisha gereza la kilimo Songwe

Sun, 26 Jun 2022 Chanzo: www.mwananchi.co.tz

Zaidi ya Sh14 bilioni zitatumiwa na kampuni ya uwekezaji ya Panda Hill kwa ajili ya kuhamisha gereza la Kilimo la Songwe  Mkoa wa Mbeya  kupisha mradi wa uchimbaji madini ya Niobium yanayotumika kutengeneza injini za ndege, magari na vyuma vya kujenga madaraja .

Mwakilishi wa  Kampuni hiyo, Emmanuel Kisasi amesema hayo leo  Jumapili June 26,2022 wakati wa Kongamano  la wadau  wa Sekta ya Nishati na Madini lililoliandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Juma Homera na kufunguliwa na Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Saimon Mayeka.

Kisasi amesema nyumba 120 za Jeshi la Magereza na  wafungwa 600 watahamishwa kupisha mradi huo.

''Tayari hatua za awali tumeanza na sasa tupo kwenye mazungumzo na Serikali ili kuanza utekelezaji wa mradi  ambao utatoa ajira 850 na asilimia 54 za manunuzi ya bidhaa yatafanyika  nchini” amesema

Ameeleza mkataba wa uchimbaji wa madini hayo utadumu kwa miaka 30 huku Serikali ikitarajia kupata   mapato ya Dola 600 milioni kwa mwaka.

Kwa upande wake Kamishna msaidizi wa Magereza na Mkuu wa Magereza Mkoa wa Mbeya , Adriano Mduda amekiri kuwepo kwa uwekezaji huo na kubainisha kuwa hautoathiri katika eneo la  mashamba yanayozalisha mazao na ufugaji katika eneo hilo la gereza.

Akifungua Kongamano hilo Mkuu wa Wilaya ya Chunya,  Saimon Mayeka amesema lengo ni kujenga uelewa wa pamoja na kuhamasisha mtandao wa kibiashara ndani na nje ya nchi ikiwa ni pamoja na kubaini changamoto zinazowakabili na kuzitatua.

Naye, Katibu Tawala Msaidizi uchumi na uzalishaji mkoani humo ,Said Madito amesema wamelenga Sekta ya Nishati na Madini kutokana na mchango wao mkubwa.

Chanzo: www.mwananchi.co.tz