Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Serikali yatoa bilioni 50 kununua mahindi

Mahindi Serikali yatoa bilion 50 kununua mahindi

Fri, 10 Sep 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Serikali imetoa shilingi bilioni 50 kwa ajili ya kununua mahindi kutoka kwa Wakulima wa maeneo mbalimbali nchini.

Haya yamebainishwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati akiahirisha mkutano wa nne wa Bunge leo Agosti 10 ,2021 jijini Dodoma na kuongeza kuwa ununuzi huo unatarajiwa kuanza jumatatu ya Septemba 13, 2021.

Waziri Mkuu, amesema fedha hizo zitatolewa kwa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA), ambao umekuwa ukifanya kazi hiyo ya kununua mahindi ya Wakulima. Aidha, Amesema Rais Samia Suluhu Hassan ameridhia kutolewa kwa kiasi hicho cha fedha baada ya kusikia kilio cha Wakulima wa maeneo mblimbali nchini kuwa mahindi yao yamekosa soko.

Bunge limeahirishwa hadi tarehe 2 Novemba mwaka huu.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live