Menu ›
Biashara
Wed, 7 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB Ruth Zaipuna, mazungumzo yaliyofanyika jijini Dodoma.
Pamoja na mambo mengine Majaliwa amepongeza mafanikio makubwa yaliyofikiwa na benki hiyo kwa hesabu za mwaka 2023.
Kwa upande wake Zaipuna ameshukuru na kupongeza ushirikiano wanaoupata kutoka kwa Serikali pamoja na mazingira bora ya utendaji ya biashara ambayo yamechangia ukuaji wa benki hiyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live