Arusha. Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amewatuliza wamiliki wa maduka ya kubalisha fedha ambayo hivi karibuni yalifungwa, kwamba yatafunguliwa baada ya Benki Kuu (BoT) kukamilisha uhakiki.
Akizungumza leo Ijumaa Mei 18, 2019 jijini Arusha katika ufunguzi wa semina ya wanahisa wa Benki ya CRDB, Majaliwa amesema BoT inakamilisha taratibu za kutolewa vibali kwa baadhi ya maduka hayo.
"Msiwe na mashaka vibali vitatoka hivi karibuni kwa maduka maalum ili kuendelea kutoa huduma lakini pia kuna benki zinatoa huduma nzuri ya kubadilisha fedha ikiwepo benki ya CRDB,” amesema
Awali Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo ameishauri CRDB kuteua moja ya matawi yake jijini Arusha kufanya kazi hadi usiku ili kutoa huduma ya kubadilisha fedha.
Amesema Arusha ni Jiji la kitalii, ili kuondoa adha kwa watalii huduma ya kubadilisha fedha zinapaswa kuboreshwa zaidi.
Hivi karibuni BOT ka kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama waliendesha operesheni ya kufunga maduka ya kubadilisha fedha, katika majiji ya Arusha na Dar es salaam na manispaa ya Moshi na kusababisha adha kwa watu kwa wananchi na wageni.
Habari zinazohusiana na hii
- Serikali ilichobaini maduka ya kubadilisha fedha
- VIDEO : Tanzania yafafanua masharti ya kusafirisha dola
- Mazito yaibuka ukaguzi wa maduka ya fedha za kigeni
- VIDEO : Serikali Tanzania yajivunia akiba ya fedha za kigeni