Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Serikali ya Tanzania yaridhishwa ujenzi mradi wa umeme wa kilovoti 400

67912 Umeme+pic

Tue, 23 Jul 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Arusha. Serikali ya Tanzania imesema imeridhishwa na mkandarasi wa mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa kilovoti 400 yenye urefu wa kilomita 414 inayopita Mikoa ya Singida, Manyara, Arusha hadi Namanga.

Mkandarasi huyo, Kenya-Tanzania Power Interconnection (KTIPIP) ZTK ilianza kujenga njia hizo mwaka 2017 na kutarajiwa kumaliza Aprili, 2010.

Ujenzi huo unagharimu zaidi ya Sh600 bilioni, hadi sasa umetekelezwa kwa asilimia 51.

Hayo yameelezwa leo Jumanne Julai 23, 2019  na kamishna wa nishati jadidifu, Innocent Luoga wakati akihitimisha  ziara yake ya siku mbili ya  kukagua ujenzi huo.

Katika ziara hiyo, amekagua njia ya umeme ya Namanga ,kituo cha kupoozea umeme cha Legur  kilichopo halmashauri ya Wilaya ya Arumeru  pamoja na njia  za kusafirishia umeme zilizopo katika halmashauri ya Babati vijijini.

Amesema hadi sasa wameshasimamisha minara zaidi ya  100 kati ya 384 inayotakiwa.

Pia Soma

Mratibu na msimamizi wa mradi huo kutoka Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Peter Kigadye amesema Serikali itawasaidia kutoa vifaa vyao vya ujenzi bandarini kwa wakati.

Mkazi wa kata ya Makuyuni, Peter Mollel ameishukuru Serikali kwa kuwapatia mradi huo, kuomba uharakishwe ili kuleta maendeleo katika eneo hilo, ikiwa ni pamoja na kuanzishwa viwanda vidogo.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz