Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Serikali ya Tanzania yaeleza inavyovutia wawekezaji

Serikali ya Tanzania yaeleza inavyovutia wawekezaji

Mon, 3 Feb 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Serikali ya Tanzania itaendelea kuvutia uwekezaji katika maeneo yote yenye rasilimali ikiwemo Jasi inayopatikana katika kata za Bendera na Makanya wilayani Same Mkoa wa  Kilimanjaro.

Hayo yameelezwa leo Jumatatu Februari 3, 2020 na Waziri  Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji),  Angella Kairuki wakati akijibu swali la Mbunge wa Same Mashariki (Chadema) Naghenjwa Kaboyoka.

Kaboyoka amesema kata za Bendera na Makanya zina Jasi nyingi na zinaweza kutoa malighafi kutengenezea Gypsum boards, mabomba ya maji machafu, saruji, POP na mbolea.

“Serikali ina mpango gani wa kusaidia kupatikana kwa

mwekezaji ili aanzishe viwanda hivyo katika maeneo hayo wilaya ya Same,” amehoji.

Akijibu swali hilo, Kairuki amesema azma ya Serikali ni kujenga uchumi wa kati unaoongozwa na sekta ya viwanda ifikapo mwaka 2025.

Pia Soma

Advertisement

Amesema viwanda vinavyotumia rasilimali zinazopatikana nchini na kuzalisha bidhaa zinazotumika kwa wingi vimepewa kipaumbele.

“Kutokana na utekelezaji wa azma hiyo, nchi yetu sasa imeweza kuzalisha baadhi ya bidhaa zinazotosheleza soko la ndani na ziada kuuza nje ya nchi ikiwemo bidhaa zinazotokana na malighafi ya jasi,” amesema.

Amesema lengo la Serikali ni kuongeza uzalishaji wa ndani na kupunguza uagizaji wa bidhaa kutoka nje katika maeneo yote yenye rasilimali zinazoipa Tanzania faida ya ushindani.

Chanzo: mwananchi.co.tz