Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Serikali ya Tanzania kutumia bidhaa ya Kiswahili kufikia uchumi wa viwanda

75763 Tzpic

Mon, 16 Sep 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Arusha. Serikali ya Tanzania imesema itatumia Kiswahili kama bidhaa katika kufikia azma ya uchumi wa  viwanda.

Akizungumza wakati wa kufunga maadhimisho ya Kitaifa ya Kiswahili na Utamaduni leo Jumamosi Septemba 14,2019 jijini Arusha, mgeni rasmi Naibu Waziri wa  Viwanda na Biashara nchini Tanzania, Stella Manyanya amesema Serikali itasimamia lugha ya Kiswahili kufanikisha azma ya kufikia uchumi wa  viwanda.

Amesema Serikali ya awamu ya tano imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kinatumika kwa mawanda mapana kwenye Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika.

"Ninampongeza Rais wetu Dk John Magufuli ameleta msukumo mpya katika kukuza na kuendeleza Kiswahili," amesema Injinia Manyanya.

Katibu Mtendaji Baraza la  Kiswahili la  Taifa (Bakita), Dk Selemani Sewangi amesema maadhimisho ya kitaifa yatakuwa yakifanyika kila mwaka kama ilivyokuwa awali miaka kumi iliyopita.

Mwenyekiti wa  Baraza la  Kiswahili Zanzibar (Bakiza), Dk Mohammed Seif Khatib amesema mabaraza ya Kiswahili yataendelea kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuendelea kuenzi muungano wetu.

Pia Soma

Advertisement
Amesema linapotokea jambo ambalo linahusu kimataifa Bakita iwashirikishe wenzao wa  Zanzibar.

Akizungumza kwa niaba ya vyombo vya habari, Charles Hillary amesema Bakita itumie kanuni zake mpya kutoa mafunzo kila mwezi kwenye vyumba vya habari.

Pia, amesema katika sherehe za kitaifa kumekuwa na nishani zikitolewa kwa makundi mbalimbali lakini ni  wakati mwafaka kuanza kutambua mchango wa  vyombo vya habari hasa katika kukuza Kiswahili.

Chanzo: mwananchi.co.tz