Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Serikali ya Tanzania kununua ndege kubwa ya mizigo

88573 Ndege1+pic Serikali ya Tanzania kununua ndege kubwa ya mizigo

Mon, 16 Dec 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Mwanza. Serikali ya Tanzania inapanga kununua ndege ya mizigo itakayosafirisha shehena ya bidhaa za maua na mbogamboga kwa lengo la kuongeza fursa za uwekezaji na biashara kwa wakulima nchini humo.

Mapango huo unaokusudia kuongeza na kuimarisha sekta ya usafirishaji kwa njia ya anga ndani na nje ya Tanzania utawezesha safari za moja kwa moja za bidhaa hizo kwenda na kutoka nje ya nchi.

Hayo yamesemwa na Rais wa Tanzania, John Magufuli leo Jumamosi Desemba 14, 2019 katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza kunakofanyika shughuli ya mapokezi ya ndege aina ya Bombardier Q-400 inayotoka nchini Canada.

Amesema mikakati hiyo ndiyo maana Serikali inajenga vyumba vya barafu vya kuhifadhi maua na mbogamboga katika uwanja wa Mwanza, Songwe na Mbeya.

“Mkakati pia unaendelea wa kukarabati chumba cha kuhifadhi mbogamboga na maua katika uwanja wa ndege ya Kilimanjaro,” amesema Rais Magufuli

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli ametoa ofa ya kusafiri bure kwa wajumbe wa kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) waliokutana jijini Mwanza juzi na jana kwenda Dar es Salaam na Zanzibar kesho Jumapili saa 3 asubuhi.

Chanzo: mwananchi.co.tz