Waziri wa Nishati, January Makamba leo amewasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2023/2024 ambapo moja ya mambo aliyoyasema kwenye hotuba yake ni kwamba Serikali tayari imekamilisha uandaaji wa Mwongozo na Kanuni za Utoaji Mikopo kwa Waendelezaji wa ujenzi wa Vituo vidogo vya mafuta Vijijini.
Waziri wa Nishati, January Makamba leo amewasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2023/2024 ambapo moja ya mambo aliyoyasema kwenye hotuba yake ni kwamba Serikali tayari imekamilisha uandaaji wa Mwongozo na Kanuni za Utoaji Mikopo kwa Waendelezaji wa ujenzi wa Vituo vidogo vya mafuta Vijijini. “Fursa za mikopo husika zimetangazwa na Waombaji wanatakiwa kuwasilisha maombi hadi kufikia tarehe 30 Agosti, 2023”