WIZARA ya Kilimo imesema Desemba mwaka huu mnada wa majani ya chai utafanyika katika Bandari ya Dar es Salaam.
Hayo yamethibitishwa na Naibu Waziri Hussein Bashe, ambapo alisema kuwa awali mnada huo ulikuwa ukifanyika Mombasa nchini Kenya.
“Mnada wa majani ya chai katika Bandari ya Dar es salam utaondoa madalali na propaganda zilizokuwa zinafanywa na mataifa ya kigeni kubeza chai yetu na hii itaongeza bei katika soko, tija kwa mkulima na mwonekano chanya katika mataifa ya kigeni,” alisema.
Aidha amewasihi wakulima waendelee kujiunga katika vyama vya ushirika vya wakulima ili kuongeza uzalishaji.