MBUNGE wa Viti Maalum (CHADEMA) Esther Matiko ameitaka serikali kufanya uchunguzi wa mbolea inayoingizwa nchini ili kubaini kiasi halisi kinachohitajika kwa kuwa kunataarifa za mbolea hiyo kutumika katika migodi.
MBUNGE wa Viti Maalum (CHADEMA) Esther Matiko ameitaka serikali kufanya uchunguzi wa mbolea inayoingizwa nchini ili kubaini kiasi halisi kinachohitajika kwa kuwa kunataarifa za mbolea hiyo kutumika katika migodi. Naibu Waziri wa Kilimo, Anthony Mavunde amesema Serikali itashirikiana na Wizara ya Madini kufanya uchunguzi kuhusiana na jambo hilo na kwamba serikali imeendelea kuchukua hatua kuboresha upatikanaji wa mbolea ikiwemo matumizi ya mbolea asili.