Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango amesema serikali itaendelea kushirikiana na wadau wa sekta ya madini nchini ili kuongeza tija na pato la Taifa
Makamu wa Rais amezungumza hayo leo wakati akifungua Mkutano wa Kimataifa wa uwekezaji sekta ya Madini unaofanyika kwa siku mbili katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam
Aidha Makamu wa Rais amemtaka Waziri wa Madini Doto Biteko kuhakikisha anatatua na kushughulikia changamoto zilizopo katika sekta hiyo
Mkutano huo unatarajiwa kumalizika kesho huku wadau mbalimbali katika sekta ya madini wakipata fursa ya kuonesha bidhaa zao katika mabanda yaliyopo katika ukumbi huo