Biashara

Habari

Burudani

Michezo

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Serikali, Total kufanya utafiti wa mafuta Tanzania

Thu, 16 May 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Serikali kwa kushirikiana na kampuni ya mafuta ya Total imesema itafanya utafiti wa mafuta nchini ili kuongeza kasi ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati kwa kutegemea kiwango cha mafuta kitakachogunduliwa.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Nishati Medard Kalemani wakati wa hafla ya kuwapongeza wafanyakazi na wadau wa kampuni hiyo ya mafuta katika maadhimisho ya miaka 50 ya kampuni hiyo hapa nchini inayoadhimishwa wiki nzima kwa shughuli mbalimbali jijini Dar es Salaam.

Kalemani alisema kuwa tafiti zinaonyesha kila mahali ilipogunduliwa gesi asili chini yake kuna mafuta hivyo Serikali imeanza mazungumzo na kampuni hiyo ili kufanya utafiti wa mafuta nchini.

Hata hivyo Kalemani amewataka Watanzania kuionyesha ushirikiano kampuni hiyo ambayo alisema ni mshirika muhimu katika maendeleo ya nchi.

“Naipongeza kampuni hii kwa kazi inazozifanya nchini ikiwemo  kuchangia maendeleo ya taifa, kutoa ajira za kudumu na za muda kwa Watanzania, kusambaza nishati mbadala ya jua, kuchangia huduma kwa jami pamoja na ujenzi wa bomba la mafuta la Uganda,” amesema Kalemani.

Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa Total Tanzania, Tarik Moufaddal amesema katika kipindi cha miaka 50, kampuni ya Total imefanya makubwa kwa kutoa huduma mbalimbali kwa jamii kwa lengo la kuhakikisha taifa linasonga mbele.

Pia Soma

Sherehe za maadhimisho hayo zilizinduliwa wiki iliyopita na Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa, ambapo pamoja na mambo mengine, aliwakabidhi zawadi mbalimbali wafanyakazi wa muda mrefu wa kampuni hiyo nchini na wadau wengine.

Chanzo: mwananchi.co.tz