Menu ›
Biashara
Fri, 21 Jan 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mkuu wa Mkoa wa Geita, Rosemary Senyamule amewataka wananchi wanaopata mafunzo mbalimbali ya biashara na ujasiriamali kuhakikisha wanakamilisha mchakato wa usajili wa biashara zao ili watimize vigezo vya kupewa tenda kwenye Mgodi wa dhahabu wa Geita GGML.
Mkuu wa Mkoa ametoa kauli hiyo wakati akifungua mafunzo yaliyowakutanisha wafanyabiashara mkoani humo ambayo yameandaliwa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji wa wananchi Kiuchumi (NEEC) kwa ushirikiano na mgodi wa GGML.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live